Header Ads

click here

IGP SIRRO AFANYA ZIARA KIBITI.

IGP Sirro ametuma salamu hizo wakati akizungumza na waandishi wa habari wilayani humo mara baada ya kumaliza mazungumzo na wazee wa wilaya ya Kibiti kwa kuwataka wakazi wa eneo hilo wasiwe na hofu kuhusiana na matukio ya uhalifu yanayoendelea kwa kuwa yeye mwenyewe ameamua kuingia mzigoni.

Nitume tu salamu kwao, waendelee tu kukimbia, waendelea kufanya wanayoyafanya lakini mwisho wa siku tutawarudisha kwenye mstari kwa sababu kikubwa umoja wetu ndiyo nguvu yetu. Mimi nipo mzigoni nawaomba mtupe muda uchunguzi ufanyike maana mauaji tokea zamani yapo yanaweza yakawa ya visasi ama namna nyingine kwa hiyo wana kibiti au wana Rufiji wasije wakaona mauaji mengine ya  kawaida yakawatia mashaka, mauaji toka tunazaliwa yamekuwepo kikubwa ni kwamba watupe nafasi tuweze kuchunguza tujue ni nini. Wazee wetu wa kibiti wametueleza taarifa nyingi sana na mnavyojua hawa wahalifu wanaishi ndani ya kibiti, ndani ya Ikwiriri kwa hiyo wazee wetu wamejaribu kutueleza ni wapi tunaweza kuwapata na chanzo cha mambo yote haya“ alisema IGP Sirro

Pamoja na hayo IGP Sirro amewahakikishia watanzania kuwa kibiti na maeneo mengine ya Rufiji yapo salama kabisa wala hakuna matishio makubwa kama watu wanavyoaminishwa.

“Ni wahakikishie watanzania kwa ujumla kibiti na maeneo mengine ya Rufiji siyo matishio makubwa kama watu wanavyofikiria ni maeneo yanayopitika watu wanaishi vizuri ni ile hofu iliyokuwepo tumekuja kuangalia hakuna sababu ya kuwa na hofu hala ni kakundi kadogo kana watu wachache ambao wamebadilika kuwa shetani sasa dawa ya shetani tunaijua dawa yake , namna ya kumshughulikia kama shetani” alisisitizia IGP Sirro

No comments

Powered by Blogger.